Pages

Saturday, May 18, 2013

Msigwa ‘amtunishia msuli’ Kanali Kinana Share bookmark Print Email Rating

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa 

 

 Siku mbili baada ya Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, kumtaka Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa kufuta kashfa dhidi yake, mbunge huyo ameibuka na kusema kamwe hatafuta kauli hiyo aliwahi kuitoa bungeni na katika mikutano ya hadhara.

Alisema ana ushahidi wa kutosha kuthibitisha tuhuma dhidi ya mtendaji huyo mkuu wa CCM.

Mchungaji Msigwa aliwahakikishia wapigakura wake kuwa hana hofu juu ya msimamo huo na kwamba yuko makini kwa kila anachokifanya.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Mashine tatu katika Manispaa ya Iringa juzi, mbunge huyo alisisitiza kuwa tuhuma hizo ni za kweli.

Alisema tuhuma hizo alikuwa amezitoa bungeni lakini pia katika mikutano mbalimbali ya hadhara na kwamba ana ushahidi nao.

Alisema siku 21 zilizotolewa na Kinana kupitia kwa wakili wake Erick Ng’maryo kumtaka afute kauli hizo, ni chache na kwamba yeye yupo tayari kwenda mahakamani wakati wowote kuanzia sasa.

“Nilipotoa hotuba yangu bungeni nilimtuhumu Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuwa anahusika na matukio ya ujangili ya uwindaji wa wanyamapori wakiwemo tembo hapa nchini. Sasa katibu huyo amenipa siku 21 nifute kauli yangu na nimwombe radhi, mimi ninasema siombi radhi nasubiri wito kwa kwenda mahakamani,”alisema Msigwa.

“Kinachonisikitisha zaidi wametoa taarifa hiyo kama maelezo makubwa ya kujisafisha kwenye gazeti huku mimi wala ofisi yangu ikiwa haijapatiwa barua yoyote,”alisema.Alisema hadi kufikia jana, alikuwa hajapata barua rasmi kutoka kwa wakili wa Kinana kumtaka aufite tuhuma hizo.



No comments:

Post a Comment