Pages

Thursday, May 16, 2013

Mchungaji Msingwa alia upendeleo TBC

MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), amehoji ni lini serikali itarekebisha mwonekano ulioanza kujitokeza kwa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) kwa kutoa habari kwa kukipendelea Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kwa kuwa wakati wa uongozi wa Tido Mhando TBC ilionekana kama ndege ambayo inapaa na kuwafanya Watanzania wengi kujenga imani na chombo hicho kwa maana ya kupata habari za uhakika na zisizo na upendeleo…

“Lakini kwa sasa shirika limekuwa kama ndege ambayo inarudi chini kutokana na kushindwa kutoa habari kama ilivyokuwa awali na sasa imekuwa ikitangaza habari za upendeleo wa kukibeba chama tawala (CCM). Je, serikali ina kauli gani kwa wananchi kuwa sasa wataanza kujenga imani na chombo hicho ambacho kimeishaanza kupoteza imani kwa wananchi?” alihoji mchungaji Msigwa.

Katika swali la msingi, Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Abdulla Amour (CUF) alitaka kujua ni mikoa mingapi inakosa matangazo ya TBC hadi sasa.

Aidha, alitaka kuelewa serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha shirika hilo linasikika kwa kurusha matangazo yake nchi nzima.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amoss Makala, alisema si kweli shirika hilo linatangaza habari zake kwa kukipendelea Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Makala alisema mikoa ambayo haipati matangazo ya redio ni tisa ambayo ni Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Mjini Magharibi, Kaskazini Pemba, Kusini Pemba, Geita, Mtwara, Njombe na Simiyu.

No comments:

Post a Comment