Pages

Saturday, May 18, 2013

RAIS DKT. JAKAYA MRISHO KIKWETE ATEMBELEA KIWANDA CHA EAST COASTS OILS AND FATS KAMPUNI TANZU YA METL IKIWA NI KAMPENI YA KUHAMASISHA LISHE BORA NCHINI.


Afisa Mwajiri wa kampuni ya East Coasts Oils and Fats ambayo ni Kampuni tanzu ya MeTL Bw. Eric Buberwa akisalimana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mara baada ya kuwasili katika kampuni hiyo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiendelea kusalimiana na wadau mbalimbali wa masuala ya Lishe.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiteta jambo na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakati wakielekea sehemu ya kiwanda cha East Coasts Oils and Fats. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq.

Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan akifafanua jambo kwa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kabla ya kukumimina Virutubishi vya Vitamini A katika Kinu cha kuzalisha mafuta kiwandani hapo ikiwa ni ishara ya kuhamasisha Lishe bora kwa walaji.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimimina mafuta ya virutubishi katika kinu cha kutengeneza mafuta ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Kampeni ya kuhamaisha Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani, wakati alipotembelea Kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho ni kampuni tanzu ya MeTL kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam. Wanaoshihudia tukio hilo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq (kushoto), Afisa Mkuu Mtendaji wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL Bw. Vijay Raghavan ( wa pili kushoto), Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (wa tatu kushoto) pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwahutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL mara baada ya kumaliza zoezi la kutembelea kampuni hiyo inayozalisha bidhaa mbalimbali ikiwemo mafuta ambapo amempongeza Mh. Mohammed Dewji kwa kutengeneza ajira kubwa kwa Watanzania kupitia kiwanda chake.
Baadhi ya wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL wakimsikiliza Mh.Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa kwenye picha ya pamoja na Uongozi wa Kampuni ya MeTL pamoja na wadau wa masuala ya lishe alipotembelea Kiwanda cha East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL katika Kampeni ya Uongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mkewe Mama Salma Kikwete, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq, Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), Mkuu wa Wilaya ya Temeke Sophia Mjema kwenye picha ya pamoja na wadau wengine wa masuala ya Lishe.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb) (kushoto) mara baada ya kuhutubia wafanyakazi wa Kampuni ya East Coasts Oils and Fats Kampuni Tanzu ya MeTL. Wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadiq na mdau wa masuala ya lishe.
Mkurugenzi Mkuu wa Makampuni ya MeTL Mh. Mohammed Dewji (Mb), akiagana na Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kumaliza ziara yake katika kiwanda cha EAST COAST OILS & FATS ambacho kampuni tanzu ya MeTL ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni ya Uhamasishaji wa Lishe bora kwa walaji kwa kuongezaji wa Virutubishi vya Vitamini A katika Vyakula vinavyozalishwa viwandani.

No comments:

Post a Comment