Pages

Saturday, May 18, 2013

WARAKA MAALUMU KUTOKA KWA BEN POL


Ndugu Mtangazaji fetty

            

YAH; MAJIBU YA MASWALI YA WADAU KUHUSU BEN POL LOVE CD AMBAYO NILIAHIDI KUITOA MWEZI ULIOPITA.

Husika na kichwa cha barua hapo juu, Mimi ni mwanamuziki wa Kizazi kipya ninayefanya shughuli zangu za Muziki hapa hapa jijini Dar ES salaam

          Nilianza kufanya shughuli za Kimuziki mnamo mwaka 2010 na kufanikiwa kutoa vibao Kama Nikikupata, Number 1 fan, Samboira nakadhalika, na hiyo ilinipelekea kujizolea mashabiki lukuki, na ninamshukuru Mungu maana pia nilifanikiwa na kutoa Albamu ya kwanza (Maboma) iliyotoka mwezi Februari mwaka 2011 na kusheheni vibao vinavyopendwa na kunifanya kupata mialiko mbalimbali na kupata japo Riziki.

            Mnamo mwezi Aprili mwaka 2013 nilitangaza kuwa ningetoa "CD" yangu ya Pili niliyoipa jina la "Ben Pol Love CD" ambayo ingesheheni nyimbo 18, na tayari maandalizi yalikuwa katika hatua za mwisho kukamilika.

        Ninasikitika na ninaomba radhi kwamba nilishindwa kufanya hivyo kwa wakati, na hiyo ilitokana na shughuli za upigaji picha wa video ya wimbo wangu mpya "Jikubali" ambayo niliifanyia Jijini Arusha na kunigharimu muda mwingi na gharama kuliko ilivyotarajiwa hapo mwanzoni, hivyo kunilazimu kusitisha shughuli zote kwa muda ili kufanya jambo moja kwa nafasi zaidi.

        Napenda nikuahidi Mtanzania mwenzangu pia Shabiki na Mdau wa muziki kwamba "Ben Pol Love CD" iko pale pale na itatoka, tarehe na mwezi wa kuitoa nitaitangaza hivi karibuni mara tu baada ya kupata Video ya Jikubali na kui-schedule kwamba nayo inatoka lini.

       Mwisho napenda kukushukuru kwa kusikiliza barua yangu, na kwa mchango wako katika muziki wangu.

   Kwa sasa kuelekea kwenye kilele cha Utoaji wa tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards kwa mwaka 2013, unaweza kuniwezesha kushinda Tuzo katika vipengele vifuatavyo;

     Wimbo bora wa Mwaka "Pete" tuma SMS "AA5" kwenda 15345

      Wimbo bora wa RnB -Maneno Maneno SMS "BU3" kwenda 15345

      Wimbo bora wa RnB -Pete SMS "BU4" kwenda 15345

     Msanii bora wa kiume (Kiujumla) SMS "AF2" kwenda 15345

       Msanii bora wa kiume (Bongo Flavour) SMS "AB1" kwenda 15345

 Mtunzi bora (Bongo Flavour) SMS "AU3" kwenda 15345
      
   Natanguliza shukrani zangu za dhati, 
  Wako katika ujenzi wa Taifa,
                    BEN POL
                 Benard Paulo 
           Dar ES salaam, Tanzania

No comments:

Post a Comment