Pages

Saturday, May 18, 2013

POLISI AKUTWA AMEKUFA

 ASKARI Polisi E7122 George Elias Mwakani, aliyekuwa akifanya kazi mjini Musoma, Mara, amekutwa amekufa katika eneo la mtaa wa Nyasura huku mwili wake ukiwa na majeraha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Absalom Mwakyoma, alisema askari huyo aliyekuwa na cheo cha Koplo, alitoweka kazini tangu Aprili 30 mwaka huu na kwamba tayari walikuwa wameshasambaza taarifa za kupotea kwake katika maeneo mbalimbali.

“Askari huyo alitoweka tangu Aprili 30 mwaka huu na tulikuwa tumeshatoa taarifa hadi jana nilipopata taarifa za kifo chake lakini tunaendelea kufanya uchunguzi wa kifo chake,’’ alisema.

Akizungumza na Tanzania Daima, mdogo wa marehemu, Abel Elias, alisema kaka yake alionana naye mara ya mwisho mwezi uliopita akiwa kazini kwake.

Mwili wa askari huyo umehifadhiwa katika hospitali ya DDH Bunda ukisubiri kufanyiwa uchunguzi na madaktri ambao watatoa taarifa sahihi ya kifo hicho. 

Source:Tanzania daima

No comments:

Post a Comment