Kikosi Cha Bongo Movie ambacho kimewatoa Jasho Taswa Fc
Kikosi cha Taswa FC 
kilichoshikishwa Kamera na timu ya bongo movie hapo jana katika bonanza 
la taswa na bongo movie lililofanyika katika viwanja vya TCC Chang'ombe 
ambapo Bongo Movie ilishinda magoli 2 kwa 0 dhidi ya Taswa fc
Mchezaji wa Taswa FC ambaye pia 
ndio mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari Za Michezo Juma Pinto 
(Mwenye Jezi ya Blue no 16) akigombania mpira dhidi ya Mchezaji wa Bongo
 movie katika mechi ya kirafiki iliyofanyika jana katika uwanja wa TCC 
Chang'ombe ambapo bongo movie iliibuka na ushindi wa Magoli 2 kwa 0
Mchezaji wa bongo movie Steve 
Nyerere akikimbilia mpira katika mechi ya kirafiki kati ya bongo movie 
na Taswa Fc iliyofanyika jana katika uwanja wa TCC Chang'ombe, bongo 
movie iliibuka mshindi kwa magoli 2 kwa 0 dhidi ya taswa fc.
hatari langoni mwa timu ya Taswa Fc.
Refarii wa Mechi kati ya Bongo 
Movie na Taswa Fc ambaye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya Ali Kiba 
akiwa makini kufuatilia Mchezo huo wakati mtanange ukiendelea...Refa 
hapo unafanya nini sasa.... 
Mchezaji wa bongo movie akijaribu 
kumtoka beki wa Taswa Fc katika mechi ya kirafiki dhidi ya Taswa Fc 
ambapo bongo movie ilishinda magoli 2 kwa 0.
Kipa wa taswa fc alipokuwa 
akijaribu kuokoa mchomo bila mafanikio na kupelekea Bongo movie kuandika
 goli la kwanza kwa mkwaju safi.
Wachezaji wa Bongo movie wakiwania
 mpira dhidi ya mchezaji wa Taswa FC jana katika mechi ya kirafiki 
iliyofanyika katika uwanja wa TCC Chang'ombe
Timu ya Bongo Movie ikichuana 
vikali katika mchezo wa mpira wa pete dhidi ya timu ya taswa queen 
ambapo kwenye mchezo huu bongo movie walichezea kichapo cha zaidi ya 
magoli 50
Mchezaji wa Bongo Movie akijaribu 
bahati yake ya kushinda goli dhidi ya Taswa queen katika mechi ya 
kirafiki iliyofanyika jana katika uwanja wa TCC Chang'ombe katika mchezo
 wa netball bongo movie walipokea kichapo kizito kutoka kwa Taswa queen.
Mchezaji wa Bongo Movie Jackline 
Wolper akijiandaa kuingia kwaajili ya kuisaidia timu yake ambayo 
ilipokea kichapo kizito kutoka kwa waandishi wakike wa habari za michezo
 taswa queen katika mchezo wa kirafiki uliofanyika jana katika uwanja wa
 TCC Chang'ombe Temeke.
Baadhi ya waandishi wa habari 
wakifuatilia mchezo wa netball kwa makiini wakati timu yao ikichuana na 
timu ya bongo movie katika mechi ya kirafiki iliyofanyika katika uwanja 
wa TCC Chnag'ombe ambapo Taswa queen waliibuka kwa ushindi mzito dhidi 
ya bongo movie.
Baadhi ya mashabiki na waigizaji 
wa filamu za kibongo wakifuatilia mtanange wa mpira wa miguu aka soccer 
wakati timu ya mpira wa miguu ya bongo ikichuana vikali na timu ya mpira
 wa miguu ya waandishi wa habari za michezo aka Taswa fc katika mchezo 
wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa TCC Chang'ombe hapo jana na 
kupelekea bongo movie kuibuka vinara kwa kuichapa taswa fc magoli 2 kwa 
0.
 Baadhi ya wadau wa michezo 
wakifuatilia mtanange wa mpira wa miguu kati ya bongo movie na taswa fc 
uliofanyika jana katika viwanja vya TCC Chang'ombe na bongo movie 
kuibuka washindi kwa magoli 2 kwa 0
 Bloggerz
 wakiwa bize katika kumuzisha matukio. Kutoka Kushoto ni Othman Michuzi 
wa Mtaa kwa Mtaa blog, Le Mutuz William Malechela, Mwenyekiti wa Chama 
Cha Waandishi wa habari za Michezo TASWA Mh Juma Pinto, Muhidini Sufian 
 wa Sufiani Mafoto Blog, akifuatiwa na Bepari aka Lukaza the Blogger wa 
Lukaza Blog wakiwajibika. 
 
No comments:
Post a Comment